Unasisitiza kuwa dawa ya deni ni kulipa. Jamii ya Wairaqw inasisitiza haki na usawa; watu huishi kwa maadili waliyorithishwa kutoka vizazi tangu kale. Jamii inakataza kudhulumu amana isiyo ya halali. Mtu akikopa amana ya mwingine ni sharti alipe kabla hajachukuliwa hatua kwa mujibu wa jamii.