Unatoa dhamira kuwa jamii na watu waliozoea kesi muda wowote maisha yao yanaweza kuharibika kutokana na kutokuwa na uaminifu na kuingilia mambo yasiyowahusu. Mtu aliyezoea kuhalalisha ubatili mwisho wake maisha yake huharibika pamoja na familia kukosa mwelekeo. Jamii haina budi kutenda haki ili kuepusha laana, lawama, chuki, visasi na mafarakano.